Sunday, June 2, 2019
Tuesday, September 26, 2017
USINDIKAJI WA PAPAI
USINDIKAJI WA PAPAI
Papai ni mojawapo ya mazao ya matunda yenye vitamini A na madini ya kalishamu kwa kiasi kikubwa sana.
Zao
Hili hustawi kila mahali nchini Tanzania. Kwa mwaka, wastani wa tani
2,580 hadi mwaka 2016, huzalishwa kote nchini, na uzalishaji wa zao hili
unaongezeka kila msimu kulingana na uhitaji.
Matunda husindikwa ili kupata bidhaa za aina mbalimbali kama vile jamu, na matunda makavu.
NAMNA YA KUSINDIKA PAPAI ILI KUPATA JUISI
Mahitaji:
Visu vikali visivyoshika Kitu
Vyombo vya kuoshea matunda
Mashine ya Kusaga matunda
Kipimo cha Sukari
Chupa zenye mifuniko imara
Saa
Nembo na lakiri
Kipima joto
Sufuria
Jiko
Mwiko
Vitambaa au chujio
MALIGHAFI KWA AJILI YA KUTENGENEZA LITA 3 ZA JUISI
MAPAPAI mawili ya ukubwa wa kati
Sukari gramu 100
Juisi ya limao/ndimu kikombe cha Chai kimoja
Maji safi na salama Lita 3
NAMNA YA KUSINDIKA
Osha matunda kwa maji safi na salama
Menya kuondoa Mabanda na mbegu
Katakata vipande vidogo vidogo, kisha saga kwa kutumia mashine ili kupata rojo.
Ongeza
maji ya limao au ndimu ili kupata ladha. Katika Kila Lita 1 ya rojo ya
mapapai weka kikombe kimoja cha Chai cha Juisi ya limao au ndimu ili
kuongeza ladha na kuboresha uhifadhi. Ongeza maji safi kiasi cha Lita 3.
Chuja kwa kutumia chujio safi.
Chemsha mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 20 ukiwa unakoroga katika joto la nyuzi 80°C hadi 90°C
Ipua
Weka Juisi kwenye chupa safi zilizochemshwa Ikiwa na moto kisha funga kwa mifuniko imara.
Panga chupa kwenye sufuria kisha weka weka maji kufikia nusu ya kimo cha chupa.
Chemsha chupa kwa muda wa dakika 20 ili kufisha bakteria na vimelea vinginevyo.
Ipua chupa na acha zipoe
Weka nembo
Hifadhi katika sehemu safi yenye hali ya joto lisilozidi nyuzi 25°C na isiyo na mwanga mkali.
MATUMIZI
Juisi hutumika kama kinywaji au kiburudisho na ina virutubisho vya vitamini C na A kwa wingi
USINDIKAJI WA MAPAPAI KWA KUKAUSHA
Mahitaji:
Kaushio bora
Mashine ya kufungia, au jiko la mkaa, au mishumaa.
Meza safi ya Kukutia
Kisu kisichoshika Kitu
Beseni la kuoshea
Mifuko ya plastiki au chupa ya plastiki au kioo.
MALIGHAFI
Mapapai yaliyoanza kuiva
Maji ya malimao au ndimu
JINSI YA KUTENGENEZA
Osha mapapai yaliyoiva vizuri na yasiyo na magonjwa wala mikwaruzo.
Menya kwa kutumia kisu kikali kisichoshika kutu.
Katakata
kwenye kipande visivyozidi urefu wa sentimita 10 na Unene wa milimita
3. Ujizidisha ukubwa wa vipande havitakauka vizuri na kusababisha ubora
wake kushuka.
Viweke vipande hivyo ndani ya maji ya malimao au ndimu kwa muda wa dakika 1 hadi 2 ili kudumisha rangi papai na kuongeza ladha.
Panga vipande kwenye trei za kaushio
Kausha kwa muda wa siku 3 hadi 4 kutegemeana na hali ya jua.
Fungasha kwenye mifuko ya plastiki au chupa za kioo safi na uhifadhi kwenye sehemu kavu nyenye mwanga hafifu na safi.
MATUMIZI YA PAPAI
Papai lililoiva
Huliwa kama tunda
Hutengenezwa Jamu na Juisi
Hukaushwa na Kuliwa kwa kuchanganywa wenye saladi ya matunda au keki.
Hutia ladha kwenye ice cream
Papai bichi
Utomvu wa papai bichi, hutumika katika matumizi yafuatayo;
Kutengeneza peremende, dalia, urembo, na madawa ya kulainisha Tumbo.
Huwekwa kwenye nguo wakati wa kutengenezwa ili isifupike.
Hulainisha nyama.
Hulainisha ngozi.
Papai bichi pia hutengenezwa
Mboga
Achari
MAELEZO YA MSINGI KUHUSU KILIMO CHA VITUNGUUMAJI
MAELEZO YA MSINGI KUHUSU KILIMO CHA VITUNGUUMAJI
Ni
muhimu kumwagilia maji ya kutosha siku kumi za mwanzo tangu kusia mbegu
kitaluni. Vitunguu hukaa kitaluni kwa wiki 6-8 na miche ifikiapo upana
wa penseli na urefu wa sentimita 15 ni tayari kwa kuhamishiwa
shambani/bustanini.
Vitunguu
ni zao la mbogamboga na hulimwa kwa ajili ya balbu zake. Hulimwa nyanda
za baridi kwa wingi sana. Nyanda zenyewe joto Vitunguu kulimwa pia.
Tanzania Vitunguu hulimwa sana sehemu za Mang'ula, Mgeta, na Singida.
Hata hivyo vitunguu hustawi maeneo mengi ya Tanzania.
Vitunguu vinaweza kulimwa mwaka mzima endapo maji yanapatikana.
Vitunguu vina matumizi mengi sana na vina madini joto, chuma, vitamini A, vitamini B, vitamini C, na vitamini E.
HALI JOTO
Joto
linatakiwa sana kwa ajili ya ukuaji wa balbu ila joto likizidi vitunguu
hukomaa mapema kabla ya balbu hazijazifia ukubwa unaostahili, hivyo
mkulima anaweza kupata mazao kidogo.
UDONGO NA MAHITAJI YA MAJI
Vitunguu
huweza kupandwa kwenye udongo wowote wenye rutuba, usiotuamisha maji na
usionata sana. Hufanya vizuri kwenye udongo wenye asidi kidogo hapo
udongo wenye alkali kidogo sio mbaya sana. Kwenye udongo wenye mchanga
mchanga umwagiliaji ni Lazima. Udongo mzuri sana kwa ustawi wa vitunguu
ni tifutifu-kichanga.
Umwagiliaji ni muhimu sana hasa wakati wa kuanza kutengeneza balbu. Unyevu uliozidi ni hatari sana kipindi cha ukuaji.
Epuka matumizi ya mbolea mbichi isiyoiva vizuri Kwani husababisha vitunguu kuwa na shingo pana sana kipindi cha ukuaji.
UZALISHAJI NA UPANDAJI WA VITUNGUU
Kabla
ya kupanda udongo ni Lazima utifuliwe vizuri na reki kuondoa mabaki ya
mimea na mawe au kipande kikubwa vya udongo. Matuta yawe na upana wa
mita moja. Vitunguu hupandwa kwa mstari moja kwa moja au kutokea
kitaluni. Pia huweza kupandwa kwa mstari pacha. Vitunguu hupandwa
sentimita 10-15 kutoka mmea hadi mmea na sentimita 10-15 kutoka mstari
hadi mstari.
EPUKA
Kununua mbegu za mitaani, kuzidisha sana mbolea na umwagiliaji usio na mpangilio kwani husababisha vitunguu kuzaa pacha.
Epuka pia kupanda vitunguu mahali palipopandwa mboga jamii ya vitunguu siku za nyuma. Mfano vitunguu saumu au vitunguu majani.
KITALU CHA VITUNGUU
AINA YA VITUNGUU VINAVYOLIMWA TANZANIA
. RED CREOLE
. BOMBAY RED
. HYBRID F1
UTUNZAJI SHAMBA
Kutandazia
shamba na Majani yaliyooza vizuri ama mabua Inashauriwa ili kuongeza
rutuba ya ardhi, Zuia magonjwa yatokanayo na udongo na magugu. Kupanda
vitunguu kwenye matuta yaliyoinuka ni muhimu sana kuzuia utuamishaji wa
maji na milipuko ya magonjwa ya miche. Kung'oa magugu na uvunaji ufanywe
kwa mkono.
MAHITAJI YA MBOLEA
Vitunguu
hufanya vizuri kama shamba litawekewa mbolea ya samadi ama mboji
iliyoiva vizuri. Kiasi cha tani 25-40 kwa heka kina shauriwa. Hii ni
sawa na kilo 7.5-12 kwa tuta lenye urefu wa mita 3 na upana wa mita 1
UVUNAJI
Vitunguu
huvunwa kuanzia siku 90-150 tangu kusia mbegu. Dalili za kukomaa ni
kuanguka kwa Majani. Vitunguu huvunwa kwa kuvuta kwa mkono na
kuhifadhiwa siku kadhaa shambani vikiwa vimefunikwa na majani. Baada ya
hapo majani hukatwa na balbu hupakiwa kwa ajili ya kuhifadhi kusubiria
bei nzuri. Vitunguu huweza kuhifadhiwa hadi miezi 9 tangu vivunwe bila
kuharibika. Vitunguu vihifadhiwe kwenye sehemu ya nyuzi joto chini ya
4.4°C ama juu ya nyuzi joto 25°C ili visiharibike.
UUZAJI
Vitunguu
ni zao lenye bei nzuri ukilinganisha na mazao mengine ya mbogamboga na
huuzwa kwenye masoko ya kawaida kwa bei nzuri kwa hivi sasa mwezi
Septemba vitunguu kilo moja ni shilingi 1,500/= kama vitunguu vikilimwa
vizuri na kuhudumiwa ipasavyo. Hekari moja huzaa gunia 70-90 Sawa na
7,000-9,000kgs. Kama ukipata Soko la uhakika Mkulima anaweza kupata hadi
milioni 13.5 kwa Msimu mmoja.
BUSTANI YA FREBU
S.L.P. 77585, DSM, TANZANIA
Saturday, September 23, 2017
Karibu kwenye blog ya frebu media
Karibu kwenye blog ya Frebumedia blog. Blog hii inakupa habari za kweli na uhakika. Utapata habari za uhakika na matukio ya kila siku. Karibu sana frebumedia.blogspot.com blog yako ya kweli.
Ukiwa unataka kutangaza kwenye blog hii unakaribishwa. Tangaza kwa bei rahisi kuliko sehemu nyingine yoyote. Utalipia pesa ndogo sana kutangaza kwenye blog hii ys uhakika zaidi. Tunapokea matangazo ya aina yoyote iwe kutangaza blog au kutangaza huduma au biashara. wasiliana nasi kwa email hii buberwamujuni@gmail.com utajibiwa na kuwekewa tangazo lako kwenye mtandao huu bira zaidi
Saidia kushare blog hii kwenye magroup ya whatsapp facebook twitter na kwingineko Ili mamilioni ya watu waje kusoma blog hii wapate habari za kweli na uhakika. Watumie anwani ya blog hii ambayo ni frebumedia.blogspot.com mtu akibonyeza link hiyo ataletwa kwenye blog hii.
Ukiwa unataka kutangaza kwenye blog hii unakaribishwa. Tangaza kwa bei rahisi kuliko sehemu nyingine yoyote. Utalipia pesa ndogo sana kutangaza kwenye blog hii ys uhakika zaidi. Tunapokea matangazo ya aina yoyote iwe kutangaza blog au kutangaza huduma au biashara. wasiliana nasi kwa email hii buberwamujuni@gmail.com utajibiwa na kuwekewa tangazo lako kwenye mtandao huu bira zaidi
Saidia kushare blog hii kwenye magroup ya whatsapp facebook twitter na kwingineko Ili mamilioni ya watu waje kusoma blog hii wapate habari za kweli na uhakika. Watumie anwani ya blog hii ambayo ni frebumedia.blogspot.com mtu akibonyeza link hiyo ataletwa kwenye blog hii.
Subscribe to:
Posts (Atom)