Tuesday, September 26, 2017

MAELEZO YA MSINGI KUHUSU KILIMO CHA VITUNGUUMAJI

Tags

MAELEZO YA MSINGI KUHUSU KILIMO CHA VITUNGUUMAJI


Vitunguu ni zao la mbogamboga na hulimwa kwa ajili ya balbu zake. Hulimwa nyanda za baridi kwa wingi sana. Nyanda zenyewe joto Vitunguu kulimwa pia. Tanzania Vitunguu hulimwa sana sehemu za Mang'ula, Mgeta, na Singida. Hata hivyo vitunguu hustawi maeneo mengi ya Tanzania.

Vitunguu vinaweza kulimwa mwaka mzima endapo maji yanapatikana.

Vitunguu vina matumizi mengi sana na vina madini joto, chuma, vitamini A, vitamini B, vitamini C, na vitamini E.

HALI JOTO
Joto linatakiwa sana kwa ajili ya ukuaji wa balbu ila joto likizidi vitunguu hukomaa mapema kabla ya balbu hazijazifia ukubwa unaostahili, hivyo mkulima anaweza kupata mazao kidogo.

UDONGO NA MAHITAJI YA MAJI
Vitunguu huweza kupandwa kwenye udongo wowote wenye rutuba, usiotuamisha maji na usionata sana. Hufanya vizuri kwenye udongo wenye asidi kidogo hapo udongo wenye alkali kidogo sio mbaya sana. Kwenye udongo wenye mchanga mchanga umwagiliaji ni Lazima. Udongo mzuri sana kwa ustawi wa vitunguu ni tifutifu-kichanga.

Umwagiliaji ni muhimu sana hasa wakati wa kuanza kutengeneza balbu. Unyevu uliozidi ni hatari sana kipindi cha ukuaji.

Epuka matumizi ya mbolea mbichi isiyoiva vizuri Kwani husababisha vitunguu kuwa na shingo pana sana kipindi cha ukuaji.

UZALISHAJI NA UPANDAJI WA VITUNGUU
Kabla ya kupanda udongo ni Lazima utifuliwe vizuri na reki kuondoa mabaki ya mimea na mawe au kipande kikubwa vya udongo. Matuta yawe na upana wa mita moja. Vitunguu hupandwa kwa mstari moja kwa moja au kutokea kitaluni. Pia huweza kupandwa kwa mstari pacha. Vitunguu hupandwa sentimita 10-15 kutoka mmea hadi mmea na sentimita 10-15 kutoka mstari hadi mstari.

EPUKA
Kununua mbegu za mitaani, kuzidisha sana mbolea na umwagiliaji usio na mpangilio kwani husababisha vitunguu kuzaa pacha.
Epuka pia kupanda vitunguu mahali palipopandwa mboga jamii ya vitunguu siku za nyuma. Mfano vitunguu saumu au vitunguu majani.

KITALU CHA VITUNGUU
Ni muhimu kumwagilia maji ya kutosha siku kumi za mwanzo tangu kusia mbegu kitaluni. Vitunguu hukaa kitaluni kwa wiki 6-8 na miche ifikiapo upana wa penseli na urefu wa sentimita 15 ni tayari kwa kuhamishiwa shambani/bustanini.

AINA YA VITUNGUU VINAVYOLIMWA TANZANIA
. RED CREOLE
. BOMBAY RED
. HYBRID F1

UTUNZAJI SHAMBA
Kutandazia shamba na Majani yaliyooza vizuri ama mabua Inashauriwa ili kuongeza rutuba ya ardhi, Zuia magonjwa yatokanayo na udongo na magugu. Kupanda vitunguu kwenye matuta yaliyoinuka ni muhimu sana kuzuia utuamishaji wa maji na milipuko ya magonjwa ya miche. Kung'oa magugu na uvunaji ufanywe kwa mkono.

MAHITAJI YA MBOLEA
Vitunguu hufanya vizuri kama shamba litawekewa mbolea ya samadi ama mboji iliyoiva vizuri. Kiasi cha tani 25-40 kwa heka kina shauriwa. Hii ni sawa na kilo 7.5-12 kwa tuta lenye urefu wa mita 3 na upana wa mita 1

UVUNAJI
Vitunguu huvunwa kuanzia siku 90-150 tangu kusia mbegu. Dalili za kukomaa ni kuanguka kwa Majani. Vitunguu huvunwa kwa kuvuta kwa mkono na kuhifadhiwa siku kadhaa shambani vikiwa vimefunikwa na majani. Baada ya hapo majani hukatwa na balbu hupakiwa kwa ajili ya kuhifadhi kusubiria bei nzuri. Vitunguu huweza kuhifadhiwa hadi miezi 9 tangu vivunwe bila kuharibika. Vitunguu vihifadhiwe kwenye sehemu ya nyuzi joto chini ya 4.4°C ama juu ya nyuzi joto 25°C ili visiharibike.

UUZAJI
Vitunguu ni zao lenye bei nzuri ukilinganisha na mazao mengine ya mbogamboga na huuzwa kwenye masoko ya kawaida kwa bei nzuri kwa hivi sasa mwezi Septemba vitunguu  kilo moja ni shilingi 1,500/= kama vitunguu vikilimwa vizuri na kuhudumiwa ipasavyo. Hekari moja huzaa gunia 70-90 Sawa na 7,000-9,000kgs. Kama ukipata Soko la uhakika Mkulima anaweza kupata hadi milioni 13.5 kwa Msimu mmoja.

BUSTANI YA FREBU 
S.L.P. 77585, DSM, TANZANIA


EmoticonEmoticon